UMMA WAJERUHI POLISI NYAMIRA

Maafisa wa polisi katika eneo la Kimera kaunti ya Nyamira wamelazimika kutumia vitoza machozi kuwatawanya wakazi waliowashambulia kwa mawe na kuwajeruhi maafisa wawili.
Imeripotiwa kuwa maafisa wa polisi walikuwa wamefika katika eneo hilo kuwmokoa mwanamme aliyekuwa akishambuliwa na umma baada ya kudaiwa kuhusika katika mauaji.
Aidha, kioo cha gari la polisi aina ya landcruiser kimeharibiwa, huku mali ya thamani ya zaidi ya shilingi milioni 2 ikiharibiwa.
Imetayarishwa na: Antony Nyongesa
English 



















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































