#Local News

4 WAFARIKI KWENYE AJALI MIGAA, NAKURU

Watu 4 wamepoteza uhai papo hapo huku mwingine akijeruhiwa katika eneo la Migaa kaunti ya Nakuru kwenye barabara kuu ya Nakuru-Eldoret baada ya lori lililokuwa likisafirisha kuni kugongana ana kwa ana na lori jingine lililokuwa likisafirisha nyanya.

Kulingana na chifu wa Migaa Zachary Monari, watatu kati ya waliofariki walikuwa kwenye lori lililokuwa likisafirisha kuni na mwingine kwenye lori jingine.

Majeruhi anatibiwa katika hospitali moja eneo la Salgaa, wakazi wakilalamikia ongezeko la ajali eneo hilo.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

4 WAFARIKI KWENYE AJALI MIGAA, NAKURU

KEPSHA: JSS IMETUONGEZA MZIGO, TUTAMBUENI

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *