#Local News

POLISI WATOZWA FAINI KWA KUKOSA KUTOA USHAHIDI

Maafisa 6 wa polisi wametozwa faini ya shilingi 10,000 kila mmoja ama kuhudumia kifungo cha miezi 3 gerezani kwa kukosa kutoa ushahidi wao katika kesi ya mauaji inayomkabili afisa mwingine wa polisi.

Sita hao walikuwa miongoni mwa mashahidi 25 waliotarajiwa kutoa taarifa zao kotini kwenye kesi dhidi ya Ahmed Rashid aliyekuwa akihudumu katika kituo cha polisi cha pangani na anayedaiwa kuwapiga risasi vijana wawili mwaka wa 2017.

Uamuzi huo umetolewa na jaji wa mahakama ya Kibera Diana Racheal Kavedza.

Imetayarishwa na Maureen Mukhobe

POLISI WATOZWA FAINI KWA KUKOSA KUTOA USHAHIDI

WASHUKIWA 2 WAPIGWA RISASI MATHARE

POLISI WATOZWA FAINI KWA KUKOSA KUTOA USHAHIDI

MADAI YA OMTATAH YAIBUA UTATA BUSIA

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *