LIGI KUU YAREJEA
Ligi kuu ya uingereza EPL inaanza wikendi hii, huku Manchester City wakijinadi kuendeleza ubabe wao katika soka la Uingereza na Ipswich wakirejea ligi kuu.
Pazia litafunguliwa na Manchester United watakapokuwa wenyeji wa Fulham kuaznia saa nne usiku wa leo, mechi zikiwa zimesambaa kwa siku nne.
Ipswich inawakaribisha Liverpool Jumamosi kabla ya Manchester City kuivaa Chelsea Jumapili katika mechi mbili zinazovutia macho zaidi wikendi ya ufunguzi.
Arsenal watakuwa na matumaini kwamba hatimaye wataishinda Manchester City na kutwaa ubingwa, huku Manchester United wakipania kupona vidonda vya msimu jana , msimu wao mbaya zaidi tangu 1990.
Kuna mabadiliko ya sheria ya mchezaji kuunawa mpira, teknolojia ya VAR na muda wa majeruhi, pamoja na mengine.
Imetayarishwa na Nelson Andati
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































