WABUNGE KUWA NA UAMUZI WA MWISHO KUHUSU WAKENYA WALIOPEWA MSAMAHA WA USHURU KATIKA MSWADA MPYA
Wabunge watakuwa na uamuzi wa mwisho katika kubainisha ni watu gani au kampuni gani zitapewa msamaha wa kodi ikiwa mswada mpya utakuwa sheria.
Mswada wa Marekebisho wa taratibu za Ushuru, 2024, unalenga kurekebisha Sheria ya Taratibu za Ushuru (Sura ya 469B), kuruhusu wabunge kukagua Katibu wa Baraza la Mawaziri wa Hazina na Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Ushuru ya Kenya (KRA) mamlaka ya kutoa msamaha wa ushuru.
Sheria ya Taratibu za Ushuru inaruhusu mtu binafsi au kampuni kutuma maombi kwa Kamishna wa KRA kwa msamaha wa adhabu ikiwa watashindwa kulipa ada zao, na kupendekeza mpango wa malipo ya kiasi ambacho haijasalia.
Imetayarishwa na Janice Marete
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































