MAHANGAIKO YA MAFURIKO TRANS NZOIA
Familia zisizopungua 100 zinaendelea kukadiria hasara huku zikililia msaada baada ya kuachwa bila makao katika kaunti ya Trans Nzoia kufuatia mto Sabwani kuvunja kingo zake kutokana na mvua kubwa.
Familia hizo zimeachwa bila makao, huku mazao yao mashambani yakisombwa na mafuriko hayo mbali na shughuli za usafiri kutatizika.
Serikali imewataka waathiriwa kuhamia maeneo salama.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































