MCCARTHY AIONA FIFA SERIES KUWA JARIBIO MUHIMU KWA HARAMBEE STARS
Kocha mkuu wa Harambee Stars, Benni McCarthy, amesema mashindano ya Fifa Series yatakayofanyika Kigali, Rwanda, yatakuwa jukwaa muhimu la kupima kikosi chake kuelekea Mataifa ya Afrika ya mwaka 2027.
McCarthy amesema mashindano hayo yanatoa fursa adimu ya kutathmini wachezaji na mikakati dhidi ya wapinzani wa kimataifa.
Harambee Stars wataanza kampeni yao kwa mechi dhidi ya Estonia Machi 27 katika Uwanja wa Amahoro Matokeo ya mechi hiyo yataamua iwapo watakutana na wenyeji Rwanda au Grenada katika mchezo unaofuata.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 




























































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































