MADIRA YAJIPANGA KUTWA UBINGWA
Madira Girls wanakodolea macho taji la Shirikisho la Michezo ya Shule za Sekondari Afrika Mashariki (FEASSSA) litakalong’oa nanga kesho mjini Kakamega.
Kocha mkuu Eddy Wekesa ana imani kuwa shule hiyo yenye makao yake makuu Vihiga itabeba taji lao la kwanza la Afrika Mashariki licha ya kupoteza taji la taifa kwa mabingwa watetezi Butere Girls ambao waliwashangaza 1-0.
Mtaalamu huyo pia anatumai kuongezwa kwa kiungo wa kati wa Junior Starlets, Lindy Wee Atieno kutaongeza moto zaidi kwenye kikosi ambacho tayari kimejaa nyota.
Madira Walimaliza wa nne katika toleo la 2023 na Wekesa anatumai kwamba wataweza kujivunia mwaka huu.
Wanafungua kampeni yao dhidi ya Kawempe Muslim mnamo Ijumaa wakitafuta kuendeleza ubabe wao dhidi ya Upande wa Uganda baada ya kuwachapa 2-1 katika toleo la 2023.
Madira wako katika kundi A pamoja na wenzao Nasokol Girls, mabingwa watetezi St. Noa Girls SS na Kawempe Muslim SS kutoka Uganda, Alliance sekondari kutoka Tanzania na P.S.S.B Huye kutoka Rwanda.
Imetayarishwa na Nelson Andati
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































