#Football #Sports

WACHEZAJI WA MISRI WAMUUNGA MKONO SALAH

Wachezaji wa timu ya taifa ya Misri wameonyesha kuungana na nahodha wao Mohamed Salah, huku hatma yake ndani ya Liverpool ikibaki na sintofahamu kuelekea Kombe la Mataifa ya Afrika nchini Morocco.

Misri ambao ni mabingwa wa Afrika mara saba, wamepangwa Kundi B pamoja na Angola, Afrika Kusini na Zimbabwe

Salah hakujumuishwa kwenye kikosi kilichosafiri Milan kucheza dhidi ya Inter kwenye Ligi ya Mabingwa barani ulaya na ameashiria kuwa huenda asichezee Liverpool tena.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *