NYORO: SIJUI KWANINI NILIFURUSHWA
Mbunge wa Kiharu Ndindi Nyoro amesema hajui sababu ya kutimuliwa kwake kutoka wadhifa wa mwenyekiti wa kamati ya bajeti katika bunge la kitaifa, akisisitiza kuwa hajawahi kuzungumziwa na mtu yeyote kutoka mrengo wa Kenya Kwanza kuhusu wadhifa huo.
Akizungumza na wanahabari afisini mwake katika majengo ya bunge, Nyoro vile vile amedinda kuzungumzia uhusiano wake na viongozi wengine wa kisiasa, akiwataka viongozi kuangazia utendakazi kwa wananchi.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































