WALIMU WA JSS WADAI KUPEWA KANDARASI YA KUDUMU NA TSC

Walimu wa sekondari ya msingi JSS wamefanya maandamano katika kaunti mbali mbali humu nchini kushinikiza serikali kuwaajiri kwa kandarasi ya kudumu.
Kulingana na walimu hao tume ya huduma za walimu TSC imekiuka agizo la mahakama kuitaka kuwapa kandarasi ya kudumu baada ya kuhudumu kama walimu wanagenzi kwa Zaidi ya mwaka mmoja unusu
Maandamano hayo yanajiri wakati ambapo shule zimefunguliwa leo hii kwa muhula wa pili hali ambayo inatishia kulemaza mtaala wa umilisi CBC.
English 



















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































