SERIKALI YAAHIDI KUBORESHA AFYA
Huku wengi wa wakenya wakilalamikia changamoto katika bima ya afya ya Taifa Care, serikali imeanzisha mikakati ya kutatua changamoto hizo mbali na kuboresha sekta ya afya kwa ujumla.
Kwa mujibu wa naibu rais Kithure Kindiki, miongoni mwa changamoto zinazotishia ufanisi wa bima hiyo ni hatua ya wengi wa waliojisajili kukosa kulipa ada zao.
Ameyasema haya katika kongamano la washikadau wa afya jijini Nairobi.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































