ODM YAJIANDAA BILA ODINGA
Kamati kuu ya usimamizi wa chama cha ODM imeratibu kikao maalum hii leo kujadili mustakabali wa chama hicho kufuatia kifo cha aliyekuwa kinara wake Raila Odinga.
Mkutano huo utakaongozwa na kaimu kinara wa chama hicho Oburu Odinga, utafanyika katika makao makuu ya Orange House jijini Nairobi.
Inatarajiwa kwamba wajumbe wa kitaifa wa ODM watamwidhinisha Oburu kuwa kinara rasmi, baada ya wajumbe wa Nyanza tayari kumwidhinisha.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































