ZANU-PF KUONGEZA MUHULA WA RAIS MNANGAGWA
Mrengo wa Upinzani nchini Zimbabwe umepinga pendekezo la chama tawala ZANU-PF kuifanyia marekebisho katiba ili kuongeza muhula wa rais Emerson Mnangagwa kwa kipindi cha miaka 2.
Pendekezo hilo liliafikiwa Jumamosi iliyopita kwenye kongamano la chama hicho, na iwapo litapitishwa, Mnangagwa mwenye umri wa miaka 83 ataongoza hadi mwaka wa 2030.
Hata hivyo, mojawapo wa viongozi wa upinzani James Timba, amesema Zimbabwe haifai kuongozwa na maazimio yanayotokana na makangamano ya kisiasa.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































