KISUNZI CHA BARUA ZA MATABIBU
Madaktari wanagenzi waliokesha katika makao makuu ya wizara ya afya jijini Nairobi wangali katika eneo hilo wakishinikiza kupewa barua za uajiri.
Wakizungumza na wanahabari, madaktari hao wamesisitiza kwamba hawataondoka bila barua, na kutaka waajiriwe kwa awamu moja tofauti na mpango wa wizara ya afya wa kutaka waajiriwe kwa awamu mbili.
Viongozi wa muungano wa madaktari KMPDU wako katika eneo hilo kupata suluhu kwa mgomo wa madaktari hao ambao ni 1200.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































