#uncategorized

SERIKALI YALAZIMIKA KUREKEBISHA TOZO YA MATENGENEZO YA BARABARA

Data za wizara ya uchukuzi zinaonyesha Kuendelea kwa upanuzi wa mtandao wa barabara nchini, upungufu wa bajeti pamoja na mazingira ya mfumuko wa bei umeacha serikali bila chaguo ila kurekebisha juu ya Ushuru wa Matengenezo ya Barabara.

Thamani ya mali ya barabara nchini ikiongezeka hadi takriban Shilingi trilioni 4, na kuifanya kuwa mojawapo ya uwekezaji mkubwa zaidi wa umma humu nchini.

Kulingana na waraka wa kina wa Wizara ya Barabara na Uchukuzi, mazingira ya mfumuko wa bei na kushuka kwa thamani ya shilingi ya Kenya hadi dola, kumendelea kuathiri vifaa vya ujenzi vinavyotumika katika ujenzi wa barabara, nyingi zikiagizwa kutoka nje.

Hii ni zaidi ya miaka minane iliyopita kutoka mara ya mwisho kurekebishwa kwa tozo, mwaka wa 2016, ilipopanda kutoka Shilingi 12 hadi Sh18 kwa lita moja ya bidhaa za mafuta.

Ushuru huo ulitozwa Shilingi 1.5 kwa lita moja ya bidhaa za mafuta mwaka 1994, Shilingi 2 mwaka 1995, Shilingi 2.7 mwaka 1996, Shilingi 4.8 mwaka 1998, Shilingi 5.8 mwaka 1999, kabla ya kuongezeka hadi Shilingi 12 mwaka 2015, kisha Shilingi 18 kwa kila lita, ambayo tangu hapo imepitiwa kwenda juu kwa Sh7 hadi Sh25 kwa lita ya petroli na dizeli.

Hii ni pungufu kidogo kuliko pendekezo la awali la kuweka tozo hiyo kuwa Shilingi 28 kwa lita ya petroli na dizeli, ambapo serikali ilikadiria mapato ya mwaka ya RMLF yangeongezeka hadi Shilingi bilioni 129, ikizingatiwa mambo mengine yote yalibaki bila kubadilika.

Imetayarishwa na Janice Marete

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *