USAJILI WA MAKURUTU UNAENDELEA KOTE NCHINI
Zoezi la kuwasajili makurutu wa polisi yaendelea kote nchini hata hivyo katika kaunti ya Mombasa idadi ndogo imeshuhudiwa huku baadhi ya
vijana wakishindwa kushiriki baada ya kufika wakiwa wamechelewa.
Afisa anayesimamia zoezi hilo eneo la Mvita Simon Ndiwa amewataka vijana kujitayarisha mapema kwa kuhakikisha wana stakabadhi zinazohitajika kwa usajili wa makurutu.
Imetayarishwa na Jones Koikai
English 

























































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































