IPOA YACHUNGUZA KIFO CHA MFUNGWA NAIROBI

Maafisa wa polisi na mamlaka ya IPOA wameanzisha uchunguzi baada ya mwanaume mmoja aliyekuwa amekamatwa na kuzuiliwa katika celi za kamukunji jijini Nairobi kuaga dunia.
Mwanaume huyo kwa jina Mutembei alianguka na kuzirai akiwa katika celi kabla ya kukimbizwa katika hosipitali ya kitaifa ya Kenyatta kabla ya kuaga dunia.
Mtembei alikuwa amekamatwa na kuzuiliwa kwa madai ya kutoa fujo eneo la kamukunji.
Mwili wake umepelekwa katika hifadhi ya maiti ukisubiri kufanyiwa upasuaji.
Imetayarishwa na Janice Marete