NEWCASTLE YASHINDA KOMBE LA LIGI KWA KUICHAPA LIVERPOOL 2-1
Newcastle ilishinda Kombe la Ligi baada ya kuilaza Liverpool 2-1, huku Dan Burn na Alexander Isak wakifunga mabao muhimu.
Huu ni ushindi wao wa kwanza mkubwa tangu 1969 na taji lao la kwanza la ndani tangu 1955 ushindi ambao unajiri baada ya kupoteza fainali ya 2023 dhidi ya Manchester United.
Kwa Liverpool, kichapo hiki ni pigo baada ya kutolewa kwenye Ligi ya Mabingwa, lakini bado wanaongoza Ligi Kuu kwa alama 12.
Imetayarishwa na Janice Marete
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































