RUTO ATETEA SHERIA ZA MITANDAO
Rais William Ruto ametetea sheria za kudhibiti utumizi wa mitandao ya kijamii alizoidhinisha, akiwaonya wakenya anaosema wanaeneza uvumi kuhusu sheria hizo.
Kulingana na Rais, sheria hizo zinalenga kudhibiti ugaidi, mahubiri potovu na ukiukaji wa maadili ya jamii, huku akijitetea kutokana na uamuzi wake wa kutia Saini sheria hizo wakati taifa lilikuwa kwenye maombolezo ya Waziri mkuu wa zamani Raila Odinga.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































