PASSARIS AAPA KUUNGA MKONO MSWADA WA KIFEDHA

Mwakilishi wa kike katika kaunti ya Nairobi Esther Passaris amesema ataunga mkono mswada tata wa fedha wa mwaka 2024-25, na kwamba hatatishwa na mtu yeyote.
Katika video inayosambaa mtandaoni, Passaris vile vile amepuzilia mbali shinikizo ya mrengo wa Azimio kuwataka wabunge wake kuupinga mswada huo.
Amesema ni jukumu la kila Mkenya kulipa ushuru kwa maendeleo ya taifa.
Imetayarishwa na: Antony Nyongesa
English 



















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































