DIVISHENI ZA KEIYO, KAPOMBOI KUANZA HUDUMA
Serikali imepania kurahisisha upatikanaji wa huduma zake muhimu kwa wananchi katika kaunti ya Trans Nzoia kupitia kuanzishwa kwa divisheni 2 za Keiyo na Kapomboi na kata ndogo ya Teitei katika eneo bunge la Kwanza kaunti hiyo.
Tangazo hilo limewekwa wazi na Waziri wa usalama wa kitaifa Kipchumba Murkomen ambaye pia amesema serikali ina mpango wa kuweka lami kwenye barabara ya Maridadi-Kapomboi hadi Kolongolo katika juhudi za kurahisisha uchukuzi.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 



















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































