#Local News

POLISI AUAWA NAKURU, WENZAKE WAJERUHIWA

Afisa mmoja wa polisi ameuawa kwa risasi huku wenzake 2 wakijeruhiwa na watu wanaoaminika kuwa magenge ya wahalifu wakati polisi walipokuwa wakishika doria katika eneo la Free Area jijini Nakuru usiku wa kuamkia leo.

Waliojeruhiwa ambao ni maafisa wa kituo cha polisi cha Bondeni, wanaendelea kupokea matibabu katika hospitali ya Nakuru level 5.

Kamishna wa kaunti ya Nakuru Loyford Kibaara, amesema tayari washukiwa kadhaa wamekamatwa wakiwa na bunduki aina ya AK-47.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *