GAVANA KAHIGA AJIUZULU
Gavana Nyeri Mutahi Kahiga amejiuzulu kutoka wadhifa wa mwenyekiti wa baraza la magavana kutokana na shutuma dhidi yake kuhusiana na kauli zake zinazoonekana kusherehekea kifo cha Waziri mkuu wa zamani Raila Odinga.
Kupitia taarifa, Kahiga amejutia kauli zake na kuomba msamaha kwa familia ya Odinga, chama cha ODM, magavana wenzake na jamii ya eneo zima la Nyanza kabla ya kuwasilisha barua ya kujiuzulu.
Aidha, amekariri kuwa kauli hizo ulikuwa msimamo wake binafsi na wala si wa wakazi wa Nyeri.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































