MSHUKIWA ADAIWA KUWAUMA POLISI BUNGOMA
Polisi katika kaunti ya Bungoma wanatarajia kumfikisha mahakamani mshukiwa mmoja anayedaiwa kuwauma na kuwajeruhi maafisa 2 wa polisi kutoka kituo cha Namwela, waliokuwa wamekwenda kumkamata kwa tuhuma za uhalifu.
Kulingana na wakazi, maafisa 2 kati ya 3 waliokuwa wamefika nyumbani kwa jamaa huyo katika kijiji cha Sitabicha, walishambuliwa na mshukiwa aliyewauma begani na mikononi, ila afisa wa 3 akafanikiwa kumdhibiti.
Kamanda wa polisi Magharibi mwa nchi Issa Mohamud, amesema mshukiwa atafunguliwa mashtaka ya uharibifu wa mali kimaksudi, kuzuia kukamatwa na kuwashambulia polisi.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 












































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































