#Local News

KOSKEI AWAONYA MAKATIBU WA WIZARA

Makatibu wakuu wanaohudumu katika wizara tofauti watalazimika kuwajibikia visa vya ufisadi unaoripotiwa katika wizara zao.

Ni onyo iliyotolewa na mkuu wa utumishi wa umma Felix Koskei anayesema hataruhusu rais William Ruto kulaumiwa kwa visa vya ufisadi ilhali ni wakuu hao wanaosimamia shughuli za uagizaji.

Ametaka pia kuripotiwa kwa maafisa wa serikali wanaotumia visivyo fedha za umma.

Imetayarishwa na Maureen Makhobe

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *