WAFURUSHE WANAKANDARASI WAZEMBE; WAKAZI WAAMBIA SERIKALI YA KISUMU
Wakaazi wa kaunti ya Kisumu wameitaka serikali ya kaunti hiyo kuharakisha kukamilisha miradi iliyokwama katika kaunti nzima.
Wakizungumza katika ukumbi wa Kosawo katika kaunti ndogo ya Kisumu Mashariki wakati wa Huduma Mashinani inayolenga kuboresha utoaji wa huduma, wakazi hao wameitaka serikali ya kaunti kuchukua hatua dhidi ya wanakandarasi wanaochelewesha miradi hiyo, ambayo kulingana nao imewanyima fursa ya kunufaika nayo.
Imetayarishwa na Janice Marete
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































