BANDARI QUEENS YACHARAZWA 2-1

Bandari Queens FC ilipokea kichapo cha 2-1 katika mechi ya mapema ya Ligi ya Taifa ya Wanawake (NSL) Jumapili mikononi mwa Barcelona SC kwenye Uwanja wa Mombasa Sports Club.
Mabao ya Jane Njeri na Calta Wanjala kipindi cha kwanza yaliwapa wageni ushindi huku Cynthia Okwado akiipatia Bandari Queens faraja.
Kipa wa Bandari Queens Akinyi Belinda aliitwa uwanjani dakika ya kumi ya mechi hiyo, akiokoa juhudi mbili kutoka kwa Calta Wanjala na Jane Njeri ili kuwaweka watani kwenye mechi hiyo.
Imetayarishwa na Janice Marete