KHRC YATHIBITISHA KUKAMATWA KWA WATETEZI WA HAKI SITA NAIROBI
Tume ya Haki za Binadamu Kenya, KHRC, imethibitisha kukamatwa kwa watetezi sita wa haki za binadamu waliokuwa wakitoa ombi katika Ubalozi wa Tanzania jijini Nairobi
Kulingana na tume hiyo, Miongoni mwa waliokamatwa ni Frederick Ojiro, Julius Kamau, Vincent Mboya, Lichuma na Shem huku Mwanaharakati mwingine, Geoffrey Mboya, akifafanua kuwa walienda ubalozini kuonyesha mshikamano na wananchi wa Tanzania.
Kundi hilo limekuwa likiitisha uwajibikaji kufuatia madai ya mauaji ya watu wengi nchini Tanzania baada ya uchaguzi wa urais uliokumbwa na utata, ambapo Samia Suluhu alitangazwa mshindi bila upinzani mkubwa.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































