#Football #Sports

GOODISON PARK KUWAHUDUMIA WACHEZAJI WA EVERTON WANAWAKE

Uwanja wa Goodison Park utakuwa makao mapya ya timu ya wanawake ya Everton kuanzia msimu ujao, baada ya timu ya wanaume kuhamia uwanja mpya wa Bramley-Moore Dock.

Badala ya kubomolewa, uwanja huo wa kihistoria utahifadhiwa kwa ajili ya Ligi Kuu ya Wanawake. Hii itaufanya kuwa uwanja mkubwa zaidi wa soka unaotumiwa na timu ya wanawake pekee nchini Uingereza.

Awali, kulikuwa na mpango wa kuubadilisha kuwa eneo la makazi na biashara, lakini mpango huo umefutwa baada ya Everton kununuliwa na The Friedkin Group.

Imetayarishwa na Janice Marete

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *