MLALAMISHI: HARAMISHA MATUMIZI YA IKULU KISIASA
Kesi ya kikatiba imewasilishwa katika mahakama kuu ikitaka amri itolewe kuagiza kwamba matumizi ya Ikulu ya Rais kwa shughuli zenye miegemeo ya kisiasa ni kinyume na katiba jinsi ilivyo katika baadhi ya vipengee vya katiba.
Kwenye kesi hiyo, wakili Lempaa Suyianka anahoji kuwa raslimali za umma zimetumiwa kinyume na sheria kuendeleza ajenda ya chama tawala cha UDA, washtakiwa wakiwa mwanasheria mkuu, mdhibiti wa bajeti ya Ikulu, chama cha UDA na Rais William Ruto.
Mbali na agizo hilo, anataka agizo zaidi litolewe kushinikiza raslimali zote zilizotumika kwa shughuli hizo kurejeshwa.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 



















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































