WAKULIMA WA MIWA WAPINGA ‘KUVURUGIWA UTAMU’
Kundi la wakulima wanaouza miwa yao katika kiwanda cha Nzoia kaunti ya Bungoma wamepinga vikali maandamano yaliyopangwa na viongozi wanaopinga kukodishwa kwa kiwanda hicho kwa mwekezaji wa kibinafsi, wakiwataja viongozi hao kama wabinafsi.
Wakizungumza na wanahabari mjini Webuye, wakulima hao wakiongozwa na David Opala, uwepo wa kiwanda hicho chini ya serikali hakujawafaidi kwa muda mrefu, na hivyo kukodishwa kwake ni afueni kwao.
Aidha, wameelezea matumaini ya kupatikana kwa ajira kwa vijana.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 

























































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































