RAIS ASHTUMU KIFO CHA OJWANG
Rais William Ruto ameshtumu kifo cha mwanablogu Albert Ojwang akisema waliohusika wanastahili kuchukuliwa hatua pasipo kuzingatia cheo wanachoshikilia.
Rais ameitaka idara ya polisi kushirikiana na mamlaka ya kuangazia utendakazi wa polisi Ipoa katika uchunguzi kwenye kifo hicho akisema polisi wana jukumu la kulinda usalama na maslahi ya washukiwa wanapokamatwa.
Imetayarishwa na Maureen Amwai
English 












































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































