EACC IMEFELI KUKABILIANA NA UFISADI

Seneta wa kaunti ya nyandarua John Miithu ameelekeza kidole cha lawama kwa tume ya kukabili ufisadi EACC kwa madai kwamba EACC imekuwa kiungo dhaifu katika vita dhidi ya ufisadi.
Kwa mujibu wa Miithu wametuma faili 146 za ufisadi kwa EACC ila hakuna hatua zozote zilizochukuliwa dhidi ya watuhumiwa na tume hiyo huku akiwataka wahusika katika EACC kuwajibika.
Imetayarishwa na Janice Marete