#Football #Sports

MIKEL ARTETA ASEMA ARSENALI INA UWEZO WA KUINDOA REAL MADRID

Mikel Arteta hana shaka kwamba Arsenal wanaweza kuisumbua Real Madrid katika leo katika robo fainali ya Ligi ya Mabingwa.

The Gunners hawajawahi kutawazwa mabingwa wa Uropa na watakutana na washindi mara 15 katika robo fainali huko Emirates leo na huku marudiano huko Madrid wiki ijayo.

Timu hizo mbili zimekutana mara mbili pekee katika michuano ya Uropa, katika hatua ya 16 bora ya Ligi ya Mabingwa ya 2005/06 ambapo Arsenal iliibuka kidedea.

Mhispania huyo, ambaye pia alikuwa nahodha wa Arsenal,amesema Imepita miaka 20 tangu wawe na mchezo wa aina hii na ni fursa nzuri ya kujenga historia kwe mechi hiyo.

Arsenal ilifungwa katika hatua hiyo hiyo ya Ligi ya Mabingwa msimu uliopita na Bayern Munich.

Lakini Arteta, anayetarajiwa kuanza Bukayo Saka kwa mara ya kwanza katika kipindi cha zaidi ya miezi mitatu Jumanne, alisema ni wakati wa kuandika maandishi mapya.

Jurrien Timber na Ben White, ambao walicheza saa moja katika sare ya 1-1 ya Arsenal na Everton Jumamosi, wote wanatarajiwa kupatikana, huku Jakub Kiwior akitarajiwa kupangwa pamoja na William Saliba bila Gabriel aliyejeruhiwa.

Imetayarishwa na Nelson Andati

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *