#Rugby #Sports

INJERA ANA IMANI WATAREJEA KWA KISHINDO

Mchezaji maarufu wa raga ya wachezaji saba wa Kenya, Collins Injera, ameelezea imani na matumaini katika kikosi cha sasa cha vijana cha Shujaa.

Injera, anayejulikana kwa uwezo wake wa kufunga mabao mengi na mchango mkubwa katika raga ya Kenya, anaamini kuwa timu ya sasa ina talanta na uwezo wa kufanya vyema katika mashindano yajayo.

Usaidizi wake na kutiwa moyo huenda kukaongeza ari ya kikosi hicho kinapojiandaa kwa safari yao ya kurejea katika Msururu wa Saba wa Dunia wa HSBC, baada ya kushika nafasi ya tisa kwenye Michezo ya Olimpiki ya Paris inayoendelea.

Shujaa atarejea kwenye safu ya Saba Duniani baadaye mwaka huu baada ya kushushwa daraja Mei 2023.

Injera amepongeza Muungano wa Raga wa Kenya kwa kuhusisha wachezaji wa zamani kama sehemu ya usimamizi wa timu, akiwemo Andrew Amonde ambaye ni kocha wa Shujaa Strength and Conditioning.

Imetayarishwa na Nelson Andati

INJERA ANA IMANI WATAREJEA KWA KISHINDO

TALANTA YAELEKEA KUKAMILIKA

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *