“ASANTE, LAKINI HAPANA!” WAKENYA WAJIBU
Saa chache baada ya serikali kutangaza marekebisho katika mswada wa kifedha, baadhi ya viongozi na na wananchi wameonyesha kutorisshwa na hatua hiyo, wakisema baadhi ya vipengee tata vimebakishwa kwenye mswada huo.
Mojawapo ya vipengee hivyo ni marekebisho ya sheria ya ulinzi wa data ili kuipa mamlaka ya ukusanyaji ushuru KRA kufikia maelezo ya kibinafsi ya mlipa ushuru.
Baadhi akiwemo mbunge wa Mumias Mashariki Peter Salasya, wamepndekeza kutupiliwa mbali mswada huo.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































