MWENYEKITI WA IEBC ATOA ONYO KWA WAGOMBEA
Tume ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC imetoa onyo kali kwa wagombea wa viti mbalimbali katika chaguzi ndogo zilizopangiwa kufanyika tarehe 27 mwezi huu, kuwa watachukuliwa hatua kali za kisheria ikiwemo kuondolewa kwenye orodha ya wagombea iwapo watavuruga amani.
Akizungumza katika makao makuu ya IEBC hapa jijini Nairobi mwenyekiti wa tume hiyo Erastus Ethokon amekashifu visa vya utovu wa nidhamu na vurugu hasa katika maeneo bunge ya kasipul na mbeere kaskazini
Mkutano huo umewaleta pamoja viongozi wengine katika sekta ya usalama ikiwemo inspekta jenrali wa polisi Douglas Kanja na mwenyekiti wa tume ya kitaifa na uwiano na utangamano Samuel Kobia.
Imetayarishwa na Jones Koikai
English 












































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































