GACHAGUA ROHO MKONONI, HOJA YAIDHINISHWA
Ni rasmi sasa kwamba hatma ya naibu rais Rigathi Gachagua kuendelea kuhudumu katika wadhifa huo imo mikononi mwa wabunge, baada ya spika wa bunge la kitaifa Moses Wetang’ula hoja ya kumbandua Gachagua.
Kwa sasa kinachosubiriwa ni mwasilishaji wa hoja hiyo ambaye ni mbunge wa Kibwezi Magharibi Mutuse Mwengi, kuchagua siku ya kujadiliwa kwa hoja hiyo.
Akiidhinisha hoja hiyo, Wetang’ula amesema kwamba imeafikia vigezo vyote kisheria kujadiliwa bungeni.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































