KQ YAPATA FAIDA YA DOLA MILIONI 41.7
Licha ya changamoto katika sekta ya usafiri wa anga, Kenya Airways (KQ) imepata faida ya dola milioni 41.7 katika mwaka wa fedha 2024, ikitoka kwenye hasara ya dola milioni 174.6 mwaka 2023.
Mkurugenzi Mkuu, Allan Kilavuka, amesema mafanikio haya yanaashiria mabadiliko makubwa, huku shirika likiendelea kuwavutia wawekezaji wa kimkakati.
Mwenyekiti wa KQ, Michael Joseph, amesema matokeo haya yameweka rekodi mpya kwa idadi ya abiria na mapato, yakionyesha ukuaji wa shirika hilo.
Imetayarishwa na Maureen Amwayi
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































