BIASHARA YA POMBE KARIBU NA SHULE IFUNGWE
Kamishina wa kaunti ya kakamega Michael Mwangi amewataka wamiliki wa vilabu vilivyoko karibu na taasisi za elimu kuvifunga mara moja.
Akizungumza katika hafla ya elimu Mwangi amesema ni hatia ya wamiliki hao kuendesha biashara ya aina hiyo karibu na wanafunzi.
Mwangi vile vile amewataka wazazi katika kaunti hiyo kutilia maanani elimu ya wanao na kuhakikisha walifikisha umri wa kuenda shule wanapekelekwa shuleni.
Imetayarishwa na Janice Marete
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































