MADAKTARI WAONYA DHIDI YA VITISHO KIAMBU
Muungano wa madaktari nchini KMPDU umeishutumu serikali ya kaunti ya Kiambu kutokana na vitisho vyake vya kuwafuta kazi madaktari wanaogoma, wakitaja hatua hiyo kuwa kinyume na sheria na ukiukaji wa haki zao.
Kwenye kikao na wanahabari, katibu mkuu wa muungano huo Dakta Davji Atellah, ametetea mgomo huo unaoendelea akisema unalindwa kisheria.
Madaktari kwenye kaunti hiyo wanalalamikia masuala kadhaa ikiwemo kuhamishwa kiholela.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































