#Local News

MATIBABU YAENDELEA KUSAMBARATIKA NAIROBI, MARSABIT

Wakazi katika kaunti za Nairobi na Marsabit wanaendelea kutatizika kupata huduma za matibabu kwenye hospitali za umma kutokana na mgomo wa wahudumu wa afya, wanaosema hali imedorora zaidi na kuweka maisha ya wagonjwa hatarini.

Kulingana na maafisa wa muungano wa wahudumu hao wakiongozwa na viongozi wa KUCO, takribani asilimia 90 ya huduma sasa hazipatikani, huku serikali za kaunti hizo mbili zikikosa kushughulikia matakwa yao.

Maafisa wa maabara na kliniki katika kaunti ya Marsabit wamekuwa kwenye mgomo kwa siku 115.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *