SHIDA HAZIANZI LEO, MBADI ASEMA
Waziri wa fedha John Mbadi, ametetea utendakazi wa serikali ya Kenya Kwanza akisema serikali hiyo inafanya kazi bora ikilinganishwa na serikali iliyiopita.
Akizungumza katika eneo la Suba West, Mbadi amewashutumu wakosoaji wa serikali ya sasa, amekariri kuwa changamoto za kiuchumi za sasa zilishuhudiwa pia wakati wa utawala uliopita.
Aidha, amesema serikali imetoa mgao wa kutosha kufanikisha ukuaji wa sekta za kahawa na majani chai.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































