CJ KOOME ATOA HATUA 7 ZA USALAMA MAHAKAMANI

Jaji Mkuu Martha Koome ametaja hatua za usalama zitakazotekelezwa katika mahakama zote kufuatia kupigwa risasi kwa Hakimu Mkuu Monica Kivuti katika Mahakama ya Makadara.
Katika taarifa kwa vyombo vya habari Koome amesema kuwa polisi wa Mahakama kwa kushauriana na inspekta generali wa polisi watafanya msako mkali ili kuhakikisha kwamba hakuna mtu atakayefika mahakamani akiwa na silaha.
Imetayarishwa na Janice Marete