JIANDAE KWA MVUA KUBWA, UTABIRI
Maeneo kadhaa nchini yametakiwa kujiandaa kwa vipindi vya mvua kubwa wiki hii huku maeneo mengi yakishuhudia vipindi vya ukame.
Katika ripoti yake kuhusu kipindi cha kati ya leo na Jumatatu wiki ijayo, idara ya utabiri wa hali ya anga imesema maeneo kama vile Nairobi, ukanda wa Ziwa Victoria, Rift Valley na Magharibi mwa nchi yatashuhudia mvua.
Aidha, baadhi ya maeneo hasa pwani yatashuhudia upepo mkali.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































