#Sports

SIKU YA STARLETS UGANI NYAYO

Timu ya taifa ya wanawake ya soka Harambee Starlets ina imani kwamba itashinda mechi yao dhidi ya Gambia hii leo katika uwanja wa Nyayo katika mkondo wa kwanza wa mchujo wa kuwania kufuzu kwa kombe la mataifa ya Afrika ya wanawake WAFCON. 

Mlinda lango wa timu hiyo Lilian Awuor amesema  timu hiyo ina uwezo wa kukabiliana na Gambia akisema mechi hiyo ya leo ni fursa  kwa wengi wao kushiriki fainali za mataifa ya wanawake  na kuwa mchezo huo hautakuwa rahisi ila maandalizi waliofanya yatawawezesha kuvuna ushindi.

Chini ya uongozi wa kocha wao  Beldine Odemba sasa kenya inashinikiza  kurejea  katika hatua ya bara kwa mara ya kwanza tangu mwaka wa 2016 ilipocheza mara ya kwanza AFCON  NCHINI Cameroon.

Starlets watakuwa wenyeji wa mkondo wa kwanza ugani Nyayo, kabla ya marudiano siku 4 baadaye ugani Stade Lat Dior nchini Senegal kutokana na Gambia kukosa uwanja uliofikiwa viwango vya CAF.

The Gambia ambao wanaorodheshwa katika nafasi ya 124 katika jedwali la FIFA, inasaka kushiriki mashindano ya WAFCON kwa mara kwanza.

Kwa upande wao, Starlets wanaorodheshwa katika nafasi ya 140.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

SIKU YA STARLETS UGANI NYAYO

FOREST YAWAFUNIKA PORTO, VILLA YAFUNZWA

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *