KHALWALE: VUNJA BARAZA LA MAWAZIRI
Seneta wa kakamega Boni Khalwale amependekeza kuvunjwa baraza la mawaziri ikiwa ni miongoni mwa masuala anayofaa kuyatekeleza Rais William Ruto kutokana na malalamishi yaliyoibuliwa wakati wa maandamano.
Akizungumza bungeni alipokuwa akichangia mjadala, Khalwale ametaka wadhifa wa mkuu wa mawaziri ambao kwa sasa unashikiliwa na Musalia Mudavadi pia kuondolewa.
Aidha, amepndekeza kuondolewa kwa nyadhifa zisizo kwenye katiba kama vile CASs.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































