RUTO AJITETEA DHIDI YA VIONGOZI WA KIDINI

Wakati uo huo, Rais William Ruto mwenyewe amechukua jukumu la kuitetea serikali yake dhidi ya kauli za viongozi wa kidini za hapo jana kwamba serikali yake imejaa ubinafsi badala ya kuyashughulikia maslhai ya wakenya.
Akizungumza katika hafla ya kufuzu katika chuo kimoja jijini Nairobi, Rais amewataka viongozi wa kidini na wakenya kwa jumla kuzingatia ukweli wanapotoa taarifa kwa taifa.
Aidha, amewataka viongozi kupima athari za kauli zao kabla ya kuzitoa.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa