#Sports

CITY WATIA KANDARASI NA PUMA

Manchester City wametia saini kandarasi mpya ya jezi mpya na Puma yenye thamani ya pauni bilioni 1 [Ksh 178 bilioni] katika kipindi cha miaka 10 ijayo.

Upanuzi wa City wa mkataba wao na Puma unakuwa kama ushirikiano mkubwa zaidi wa kutengeneza jezi katika historia ya Ligi Kuu.

Wakiwa wamekubali mkataba wa pauni milioni 65 kwa mwaka na kampuni hiyo ya Ujerumani mwaka 2019, mpango mpya wa City unaaminika kuwa na thamani ya pauni milioni 100 kwa mwaka hadi 2035.

Miamba ya Uhispania Real Madrid na Barcelona zote zinaripotiwa kuwa na dili za jezi zenye thamani ya zaidi ya pauni milioni 100 kwa mwaka. Mkataba huo mkubwa wa City unakuja baada ya klabu hiyo kutocheza msimu wa kwanza wa 76-12.

Vijana wa Pep Guardiola walimaliza katika nafasi ya tatu kwenye Premier League baada ya kushinda taji hilo kwa misimu minne iliyopita.

Pia walipokea kichapo cha kushtukiza katika fainali ya Kombe la FA dhidi ya Crystal Palace na kutolewa katika michuano ya hivi majuzi ya Kombe la Dunia la Klabu katika hatua ya 16 bora dhidi ya Al-Hilal ya Saudi Pro League.

Imetayarishwa na Nelson Andati

CITY WATIA KANDARASI NA PUMA

TRAVERS ASAJILIWA NA EVERTON

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *